
Tell your friends about this item:
Mungu Hakopeshwi
Zainab Alwi Baharoon
Mungu Hakopeshwi
Zainab Alwi Baharoon
Riwaya ya Mungu Hakopeshwi inaelezea maisha ya familia moja ya Unguja iliyoingia katika mitafaruku na mikasa mingi. Kila kitu huwa na chanzo na khatima; basi ni nini chanzo cha mitafaruku hiyo na khatima yake ilikuwaje? Simulizi ni juu ya baba, Bw. Ahmed, mwenye hasira kali zisizo na mipaka, aliyeongoza familia yake kwa utashi wa nafsi yake, bila kujali hisia za mkewe wala wanawe. Kumbe moyoni mwake alihifadhi siri, na hiyo siri ndiyo iliyomfanya Bw. Ahmed kuwa mkali bila kiasi, ikimsukuma azuie kurejea kwa yale yaliyomfika zamani. Lakini kivuli cha historia ya maisha yake ya nyuma hakikuacha kumuandama. Riwaya hii i meandikwa kwa lugha nzuri na fasaha, kwa ufundi wa msanii makini na mwelewa wa maisha ya jamii za Kizanzibari na za mwambao kwa jumla.
Media | Books Paperback Book (Book with soft cover and glued back) |
Released | December 20, 2017 |
ISBN13 | 9789987753932 |
Publishers | Mkuki na Nyota Publishers |
Pages | 254 |
Dimensions | 129 × 198 × 16 mm · 226 g |
Language | Swahili |
See all of Zainab Alwi Baharoon ( e.g. Paperback Book )